Zabron Singers - Jubilee Lyrics

Jubilee Lyrics

Sikukuu ya vibanda imefika
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu
Tupokee mioyo yetu tumefika
Tutazitoa mali na mioyo yetu
Familia zirekebishwe
Na ndoa zirekebushwe
Wenye kutoa turekebishewe
Imani iwe imara
Masengenyo tuache hapa
Wivu tuutawale
Uzinzi tuukumee
Na upendo ukatawale
Bishara zetu, tumeziacha
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu
Mashamba yetu
Tumeyaacha
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu


Ni desturi yako toka enzi
Uzao wako ukae pamoja
Wakuabudu na kukusifu bwana
Wafue mavazi wajitakase
Wafue mavazi ya mioyo yao
Iwe upatanisho wetu na wewe


Baraka kwa atu wote
Finyanga mioyo yao
Bariki watoto wako
Wakirudi wakutukuze
Na pale walipotoa
Rudisha wajaze tele
Na hivyo walivyo navyo
Viongezeke ukaviyunze


Baba tuko kwako
Mbeba mambo yote
Beba shida zetu kwenye hii jubilee jubilee
Takasa mioyo yetu
Jinsi upendavyo
Tusitoke vile vile
Baba tutakase mibaraka tubebe


Hii ni jubilee
Bado tuko kwenye jubilee
Tubariki kwenye hili jubilee
Mibaraka ipo jubilee
Bishara zetu, tumeziacha
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu
Mashamba yetu
Tumeyaacha
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu
Na nyumba zetu, tumeziacha
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu
Watoto wetu
Bwana tumewaleta
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu
Washiriki wote, ona tuko hapa
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu
Wachungaji wetu, ona wako hapa
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu


Hii ni jubilee
Bado tuko kwenye jubilee
Tubariki kwenye hili jubilee
Mibaraka ipo jubilee
Tumekuja kukutana na wewe mungu wetu


Jubilee Video

Jubilee Lyrics -  Zabron Singers

Zabron Singers Songs

Related Songs